JICHO LA USALITI
SEHEMU HII IMEFUNGWA
Ili kuendelea kusoma sehemu hii ya hadithi, tafadhali weka password.
Password si sahihi.
SEHEMU YA PILI
NYUMBANI KWA BOSI – ASUBUHI
Nilifika nyumbani kwa bosi kwa taxi ya kukodi niliposhuka tu nilimlipa dereva nakumwambia aondoke haraka kisha nikasogea kwenye geti la nyumba na kugonga, ulinzi ulikuwa ni mkali sana,
Mlinzi: habari yako kijana (kwa sauti ya kiaskari)
Ian: salama sana afande (nikawaonesha na ishara ya kuwasalimia kwa mkono)
Mlinzi: nikusaidie nini
Ian: nahitaji kuonana na bosi,
Mlinzi huku akionesha shauku akachukua simu na kupiga mle ndani, wakati akiongea na simu nikapata sms toka kwa Robert
Sms: kaka Ian, bosi anamtoto mdogo amezaa na kimada na mtoto anaumwa sana sasa hivi kampa taarifa bosi kwa sms,
Mlinzi: bosi kasema hakujui na wala hana makubaliano na wewe,
Ian: tazama nabii wa bwana anataka kufanya yale yaliyo mema si kufanya kama afanyavyo mbwa mwitu kujeruhi kila alie mbele yake,
Mlinzi: Aroo kijana, nitakuvuruga ubongo, hebu toka hapa,
Kwa akili ya haraka haraka niliwatambua wale walinzi kuwa ni masikini sana na niwalevi, nikajua masikini na neno la bwana kulipokea ningumu pasipo ushawishi wa ugali na maneno ya kuwapa moyo, nikaona niende nao sawa.
Ian: hebu sogeeni hapa, (wakasogea) unajua bosi wenu yupo katika matatizo makubwa sana, hebu mpigieni simu tena mwambie na ujumbe wake,
Mlinzi: hebu toka huko, usije kutuharibia kazi wewe!
Nikatoa wallet yangu nakutoa noti 3 za elfu kumi kumi kisha nikawapa wagawane, haraka sana akainua simu na kumpigia tena bosi wake,
Mlinzi: haloo bosi, huyu nabii anasema anaujumbe wako wa muhimu sana,
Bosi: pumbavu wewe! Nimekwambia nipo bize sasa, hebu mfukuzeni mwizi huyo,
Ian: (nikadakia) mwambie na ujumbe juu ya ugonjwa wa mwanae,
Mlinzi: amesema ametumwa na Mungu juu ya ugonjwa wa mwanao,
Bosi: mh! Eeh, eeh mto..to yupi, hebu mlete ndani haraka
Mlinzi: sawa bosi,
Walinzi walishangaa sana sababu mle ndani hakuna mtoto wa bosi ambaye nimgonjwa,
SEBURENI - NYUMBANI KWA BOSI
Pale sebuleni walikuwepo bosi, mkewe na binti yao mmoja wamekaa wakitazama Televisheni,
Bosi: karibu kiti kijana (kwadharau lakini kwa tahadhari kubwa)
Ian: hapana bosi sitakaa kwani mimi nimtumishi na sikuzote mtumishi huongea na bwana wake akiwa amesimama kwa heshima,
Bosi: (kwa mshangao) hee! Inamaana uo ujumbe mzito sana mpaka umekaza kiuno?
Ian: bwana amenena nami jana usiku nakuniambia, yote uyafanyayo machoni pake ni mabaya sana na utapata mapigo mengi sana usipo tii agizo lake,
Wakati naongea hivyo ofisini walikuwa wakicheka sana, niliwasikia kupitia kifaa kilichofichwa ndani ya sikio langu.
Baada ya kumjibu hivyo bosi akahamaki akasimama nakunitazama kwa jazba akaona siogopi hata kidogo, akamgeukia mke wake na binti yake,
Bosi: hebu nendeni ndani haraka!
Wakainuka na kwenda ndani haraka, moyoni nilifarijika sana nikajua ushindi ulianza kunukia,
Bosi: sikia kijana, nitakuua! Usitake kuniletea michezo ya mjini sawa?
Ian: sishangai kusikia hivyo kwani ushamuua John mtara, Asifiwe mkinda na madame loveness ukihisi watakunyang’anya madaraka yako kutokana na utendaji wao wakazi kuwa bora zaidi yako.
(kwa sauti ndogo) Mungu sio babu yako, kana kwamba unaweza kumdanganya kwasababu wewe ni bosi, tazama udanganyifu unaomfanyia mke wako na watoto adhabu yake haipimiki kwenye mzani wowote ule duniani, na usipo tubu mwanao atakufa.
Bosi alionekana kupagawa sana, Robert akaniambia kupitia kifaa cha masikioni kuwa bosi katumiwa sms nyingine na wafanya biashara wa madini wanamshukuru kwa kuwasaidia kukwepa kodi kwaiyo wamemtumia fedha kiasi cha milioni 30 kwenye akaunti yake,
Bosi: umeyajuaje haya mwanaharamu wewe! (kwasauti ya kulalamika)
Ian: mimi na wewe nani mwanaharamu, hebu chukua simu yako soma sms uliyotumiwa sasa hivi kisha nipe jibu nani mwanaharamu!
Bosi akatoa simu mfukoni wakati anaisoma, taratiibu Robert akawa ananisomea na mimi ilivo andikwa, namimi nikawa naisoma kwa sauti ya juu kidogo, bosi kuona naisoma sms yake bila kushika simu yake na bila kuona aka changanyikiwa akakaa kwenye sofa.
Bosi: oooh! We ni shetani kabisa hebu nambie tena sms hii inasema je?
Ian: (nikarudia) thanx director, mambo mazuri kwetu, tumeisha weka asante yetu Bank muda si mrefu, SAM.
Bosi akazidi kulegea na kuinuka gafla kisha kunikamata shati,
Bosi: who are you? I will kill you nooooow! (kisha akaanza kuliaa kama mtoto)
Ian: damu takatifu haipotei hata baada ya kifo, kwani nitafanyika tena, lakini hukumu ya Mungu haita kuacha kamwe, tayari mwanao yu mahututi sasa
Muda huohuo kimada wake akampigia simu bosi
Kimada: halo mpenzi, mtoto anaumwa sana, nipo naye hospitali, kawekwa chumba maalumu,
Bosi: okey nakuja muda si mrefu (kwa sauti ndogo yenye hofu)
Ian: haya muage mke wako mwambie unaenda kwa kimada
Bosi: oooh me! Why this?
Aka kaa kwenye sofa tena kama mtu aliye banwa na pumzi
Bosi: nifanyaje sasa nabii wangu!
Edwin: (akajibu kupitia kifaa changu lakini nilisikia peke yangu) toa mahelaaawau tukahonge Malaya.
Ian: (nikamjibu Edwin kijanja) umenena vema
Kisha nikamwambia bosi piga magoti na ufumbe macho ili tuombe huruma ya Mungu, akatii,
Ian: bwana mungu naomba nisikilize mtumishi wako mwema, imekuwaje mtoto huyu aende hospitali kuna nini huko
Robert akajibu kupitia kifaa
Robert: hospitali wapo doja na kobba na ndio wanamuhudumia mtoto ila tumekapiga sindano ya usingizi tu ni kazima,
Ian: ooh mungu wangu mwema naomba uniambie mtumishi wako mda gani mtoto huyu atapata nafuu,
Robert: tunategemea baada ya nusu saa katakuwa kameamka pasta,
Ian: asante bwana kwa kujibu ombi langu asante sana, oriya baba oriyaa baba,
Bosi: amen, amen
Nikamwambia bosi asimame nikampa simu iliyokuwa pembeni yake nikamwambia ampigie simu kimada wake amwambie mtoto ataamka baada ya nusu saa, amchukue aende naye nyumbani ampe panadol ya maji kijiko kimoja mtoto atakuwa salama kisha wewe utamfata jioni.
Akapokea simu haraka na kufanya kama nilivo mwambia, alipo maliza nikamwambia kwa sauti ya mamlaka,
Ian: mwite mkeo hapa,
Alishtuka sana bosi, akataka kusema neno nikamuwahi
Ian: mwite mkeo hapa sasa hivi, kabla sijabadili mawazo,
Bosi: mke wangu (kwa upole)
Mke: ndio mume wangu
Bosi: nakuomba uje maramoja sebuleni,
Alipofika mke wake alikuwa amejaa hofu na butwaa kuona mumewe kawa mpole sana,
Ian: mama, natoka na mume wako tunaelekea kazini kwake alikuwa na matatizo lakini mungu amepania kumsaidia hivo tunahitaji sara zako,
Mke: ooh! Haleluyaa, asante nabii,
Bosi alishusha pumzi na kukaa vizuri akiwa hajiamini kabisa kuwa yupo salama, mke wake akanikaribisha chai, nikaona bora ninywe chai nijipongeze kidogo, wakati nakunywa chai Edwin akaanza ujinga,
Edwin: unakunywa chai badala yakwenda naye huyo boya benki acha ufala pasta,
Ian: chai ni tamu sana, heri kwangu kukaribishwa karamuni hapa,
Bosi: Ooh! Kawaida sana nabii,tunajaribu kujenga mwili, (kwa sauti ya kujibaraguza)
Edwin: kwaiyo ndo maringo yameanza sindio eeeeh?
Ian: Unapoanza kulia kulia njaa,maana yake wewe ni maskini kati ya masikini walio zaliwa na wazazi maskini,
Bosi: sijakuelewa nabii, namaana gani?
Ian: Usijari bosi wangu, kunawakati uwa naongea pia na vinyamkera nikivikemea kurudi motoni,
Edwin: haaaaa! Umesemaje? We ndezi lala ukouko leo, uwe mke watatu wa bosi.
Bosi: (bila kujua, mimi nazungumza na wezi wenzangu, yeye akawa anajichekesha chekesha, akidhani naongea nae) ooh kumbe!
Baada yakunywa chai, tukaondoka tukaenda ofisini kwake.
OFISINI – ASUBUHI
Anaonekana bosi amekaa kwenye kiti chake akizunguka zunguka, mimi nikiwa bado nimesimama, kulikuwa na utulivu sana kwani haikuwa ni siku ya kazi,
Bosi: Nabii tafadhari niambie nini cha kufanya
Wenzangu waliposikia hivyo kupitia kifaa cha ofisini waliruka kwa furaha sana
Ian: tazama, jinsi gani upendo wa Mungu unavyo kuzunguka, chamsingi unatakiwa kufata nitakayo nena nawe sasa,
Muda huohuo bosi akatumiwa sms na mke wake kuwa ZUIA RUSHWA wapo nyumbani kwake wakitaka kumhoji, wanamsubiri. Bosi alipo soma akapagawa bila kusema neno.
Ian: usiogope juu ya hao ZUIA RUSHWA kwani nao pia ni wadhambi, bwana wa majeshi atatushindia jambo hilo, baada ya muda simrefu wataondoka kwa aibu nyumbani kwako.
Kwa hofu kubwa bosi akainamisha kichwa juu ya meza ofisini kisha akainua tena na kusema.
Bosi: nisha potea mimi, kama ZUIA RUSHWA wamefika mpaka nyumbani kwangu si hatari hiyo?
Ian: simama na upige magoti hapa jirani na mimi ili niongee na Mungu kwaajiri yako tena,
Bosi akasimama haraka nakufanya kama nilivyo mwagiza ,alipofumba macho ili tusali nikakirekebisha haraka kifaa change cha ndani ya sikio na chakwenye kola ya shati (mic) ili ofisini wanisikie vizuri,
Ian: Baba mungu uliyemkuu kuliko viumbe vyote, nakuomba umtakase mzee huyu, ondoa kila laana inayomnyemelea, funga njia na milango ya jehanamu baba mtakatuifu,
Wakati nazidi kuomba na kunena kwa lugha Edwin akaongea na mimi,
Edwin: oya pasta unasali mno utaharibu sasa, kuna taarifa za uhakika kwamba Yule mtoto wa hawara sio wa bosi ni wa dreva wake.
Ili nimjibu Edwin bila kuharibu kazi nikamalizia sala kwa style hii,
Ian: Asante sana, ooh asante sana nimekuelewa vizuri ujumbe wako ni mzuri ever, kweli wewe ni mwanasayansi kati wanasayansi, IT kati ya IT, asante sanaa bwana.
Bosi: ameeeeni,
Edwin: boya we nipo kazini mimi kamshukuru bibi yako,
Nikacheka sanaa, maana nilishindwa kujizuia vituko vya Edwin, bosi kuona nacheka sana naye akacheka pia,
Bosi: Bwana ni mwingi sana wa huruma amesema atakufunulia jambo kuu sana ambalo litakufanya umtukuze bwana maisha yako yote,
Bosi: asante abii, asante sana mtumishi
Akapigiwa simu na mke wake, kwamba zuia rushwa wameondoka, wameomba msamaha kuwa walikosea nyumba, kusikia hivyo alistaajabu sana akaniona kama nabii vile, kumbe tuliwaahidi kuwapa milioni 5 ZUIA RUSHWA ili waondoke nyumbani kwa bosi,
Bosi: zuia rushwa wameondoka nyumbani, na wameomba msamaha, asante sana nabii,
Ian: hilo nijambo dogo sana, lipo kubwa zaidi hebu mwambie dereva wako amfate kimada wako na mtoto waje hapa maramoja,
Haraka sana akampigia simu dereva aliyekuwa nje nakumwambia aje ndani haraka,
Dereva: ndio bosi nimefika,
Bosi: kimbia nyumba ndogo kamlete mama na mtoto hapa ofisini,
Dereva: (kwa hofu) sawa bosi,
Kisha akampigia simu na kimada wake ajiandae haraka.
Walipofika ndani ofisini dereva na hawara wa bosi akiwa na mtoto mikononi, dereva akatoka nje haraka akabaki kimada, bosi na mimi,
Bosi: karibu mpenzi, huyu mbele yako ni nabii Ian amekuja kunitembelea,
Kimada: (kwa dharau) karibu sana, nafurahi kukujua,
Ian: huwezi kunijua mimi, kwani mimi ni bikira tangu tumboni mwa mama yangu mpaka sasa hivi,
Ofisini walicheka sana kwa jibu langu, Jane akapumua kwa nguvu wakati akicheka ikabidi Edwin na Robert wakimbie nje ya ofisi ili wakapate hewa safi,
Kimada: haaa! We kaka unaumwa nini wewe?
Bosi: nyamaaa, samahani nabii mchukulie kawaida tu,
Ian: Nijambo dogo sana hili bosi, kwani sijafikia hata tone la mateso ya bwana wetu,
Bosi: nikweli kabisa,
Nikamgeukia Yule kimada,
Ian: naomba uwambie bosi ukweli juu ya huyu mtoto,
Kimada: nini mbona sikuelewi
Ian: hunielewi kabisa? Nasema hivi mwambie ukweli bosi juu ya huyu mtoto kabla mama yako hajaanza kuumwa mpaka kufa sasa hivi,
Kimada: (huku akitetemeka) aah---ah-mim-i- aaah sijui bana lolote lile,
Muda huu wote bosi akiwa amekaa tu kama mtu aliyechoka sana, alipo jibu tu hivyo kwamba hajui, jane akampigia simu Yule kimada kwa kutuma namba ya mama yake mzazi,
Jane: haloo dada, naongea na neema?
Kimada: ndio ni mimi, we nani? mbona unatumia namba ya mama,
Jane: mimi ni nesi mama yako ni mgonjwa mahututi,
Kisha akakata simu,
Kimada: uwii, mama angu jamani anaumwa nini mbona alikuwa mzima we mkaka mchawi wewe, shetani kabisa wewe,
Bosi: sema ukweli wewe! Mimi nimesema ukweli mtoto wetu kapona, sema wewe shauri yako mama yako atakufa,
Kimada: ku..ku..sema ukweli mtoto huyu si wakwako ni wa dreva wako,
Bosi akasimama akiwa amepagawa na hasira kali akataka kumpiga kimada wake,
Ian: stop! Acha hasira bosi, haya nimatokeo ya dhambi ulizofanya, haya wewe mwanamke beba mwanao na uende naye nyumbani kwako.
Yule kimada akaondoka kwa uchungu na mwanaye, huku akilia baada ya kuondoka bosi alikuwa kama amekunywa pombe vile,
Ian: hebu nisikilize, unaye mke mzuri sura mpaka tabia hebu achana na huyo kimada, na tena ole wako umfukuze dereva wako, muache dereva na Yule kimada waendelee wewe baki na mkeo ili mlee familia.
Bosi: sawa nabii,
Ian: ok nabii, sasa zile pesa za rushwa milioni 30 inabidi uziingize kwenye akaunti ya kanisa na utoe milioni 5 tena nje ya izo milioni 30 kama asante kwa mungu, ili hizo milioni 30 tutawahudumia wenye shida.
Bosi: hakuna shida nabii wangu,
Ofisini kusikia hivyo waliruka kwa furaha sana wakampongezana na kukumbatiana, kisha bosi akaendelea,
Bosi: Asante sana nabii yote uliyoyafanya sina cha kukulipa zaidi nitakuongezea milioni 5 zako binafsi kwa kunisaidia kuniunganisha na familia yangu.
Baada ya kushukuru akanikabidhi cheki ya shilingi milioni 40, kisha tukatoka ofisini yeye na dereva wake wakakumbatiana kuonesha upendo na amani, mimi nikaingia kwenye gari ya Robert iliyokuwa ikinisubiri kisha tukaondoka kwa kasi sana huku tukiimba kwa pamoja wimbo tulio uweka kwenye gari wa kuonesha ushindii.
Umeipenda makala hii? Washirikishe wengine kupitia WhatsApp.
Share WhatsApp
Maoni ya Wasomaji
Maoni yataonekana hapa kama comments zimewashwa kwenye post hii.
Andika Comment